MSANII wa
muziki wa kizazi kipya,Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’ amewataka watanzania
kulipigia kura bonde la Ngorongoro kuwa moja ya maajabu saba ya Afrika na pia
kujenga tabia ya kutembelea vivutio vya utalii vya ndani.
Akizungumza mjini
Ngorongoro, Diamond ambaye alikuwa huko kujionea bonde hilo ambalo ni la
kipekee ulimwenguni, amesema hakuwahi kufikiria kwamba kuna sehemu nzuri ambayo
hata watanzania wanaweza kwenda kutembea na kujionea vivutio vilivyopo.
“Hii ni mara
yangu ya kwanza kufika hapa, lakini kwa kweli nimeshangazwa na jinsi palivyo
pazuri, wanyama, mito ambayo inapita huku chini, mi huwa naona kwenye
televisheni tu katika kile kipindi cha National Geography cha DSTV lakini
sikujua kama mambo haya yapo kweli kwetu.
“Nawaomba
watanzania wenzangu waweze kutembelea Ngorongoro na vivutio vyetu vya utalii
kwa sababu kuna mengi ya kujifunza, leo kama isingekuwa Afrika sidhani kama
kungekuwa na kipindi kama National Geography, na gharama za kuja huku si kubwa,
hatupaswi kuogopa, hivi ni vitu ambavyo vinawezekana kabisa suala ni
kujipanga,” amesema.
Amesema wenzetu
kutoka Ulaya wamekuwa wakijipanga kuweza kutembelea sehemu Fulani jam bo ambalo
linawafanya waweze kutembelea nchi nyingi kufanya utalii.
“Pamoja na kuja
kupunguza mawazo lakini sehemu kama hii inasaidia kuelemisha, mwito wangu kwa
watanzania wenzangu, mashule hata vyuo waweze kuja hapa, inakuwa rahisi zaidi
kumfundisha mtoto kuhusu Simba, Twiga, au bonde la Ngorongoro kwa kumuonyesha
hiki kiko hivi, nadhani kama watoto watakuwa wanasoma kwa vitendo hawawezi
kushindwa mitihani yao kwa sababu kumbukumbu inabaki kichwani kwa kile
walichokiona,” amesema.
Msanii huyo
alikwenda Ngorongoro baada ya kumalizika kwa tamasha la Fiesta ambapo alikuwa
mmoja wasanii waliofanya vizuri. Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ilimualika
Diamond huko. Ngorongoro ni moja kati ya vivutio vya Tanzania vinavyotakiwa
kupigiwa kuingia katika maajabu saba ya Afrika
0 comments:
Post a Comment