Friday, April 13, 2012

.......INI EDO ALA KIAPO CHA KUFA NA KUPONA.......


Mwigizaji huyo anasema ingawa ndoa yake ni ngumu kwa kuwa mume anaishi Marekani na yeye Nigeria, anajitahidi kwa nguvu zote kuhakikisha haiyumbi.

Siyo rahisi kuimudu ndoa ya aina hii, lakini nimejiwekea mipaka ya kazi na maisha binafsi, unapokuwa muda wa kupiga kazi nafanya hivyo na unapofika wa kuwa na mume wangu, nakwea pipa kumfuata, anasema Edo.

Anaongeza kuwa pamoja na kuwa anatumia nguvu nyingi kuifanya ndoa yake idumu, lakini anashukuru kwa kupata mume muelewa ambaye anapohisi kazidiwa na kazi huwa anamfuata Nigeria kuwa naye pamoja.

Edo ameongeza kuwa ni miaka mitatu sasa tangu afunge ndoa na mwanamume huyo kwa hiyo kilichopo katika mpango ni kutafuta mtoto na kuanzisha familia.

0 comments:

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Grants For Single Moms