Inawezekana uliwaza labda kampa mimba mwanafunzi, kaiba, kapigana? Kamtukana mtu? Hayo yote inawezekana yaliku majibu yako, na kama ndio hivyo…. Haujapatia kwa sababu ukweli wenyewe, Dully kaamua kuuweka wazi.
Dully amesema “nilikua naelekea mjini kusaini mkataba wa tangazo la pombe sasa kufika pale keko kumbe kulikua na msafara wa Rais anaelekea Airport, sasa kufika pale jamaa mwenye pesa yangu ya tangazo akasema anataka kusepa kwa hiyo akili yangu ikawa inawaza kuwahi, kumbe askari alikua amenizuia nikataka kumgonga, akawa ananizuia nikaona sasa huu umeshakua msala, ikabidi nikimbie niende keko nikakutana na foleni ikabidi niingie kwenye petrol station, nikasimama nikazima gari, nikashuka”
Dully amesema “polisi walinizingira kabla na kuanza kukoki mabastola yao, polisi wengine wakaongezeka na defender, nikashuka kwenye gari ikabidi niongee nao kwa hiyo nikawaambia mi nawahi sehemu ikabidi waniambie basi subiri msafara wa rais upite tutakuachia, hata hivyo walinikuta na makosa mawili ambayo waliniandikia, nilikua sina leseni niliacha nyumbani na kosa jingine ni insuarance yangu kuisha, hakuna kingine zaidi ya hapo”
0 comments:
Post a Comment