MTAYARISHAJI
na mwigizaji wa filamu za Bongo, Dometria Alphonce 'DD', ameingia rasmi katika
uandaaji wa filamu kwa kuandaa filamu inayohusu maisha yake halisi ya ndoa.
Msanii huyo ameamua kurekodi filamu hiyo inayoitwa 'Kua Uyaone' kama faraja kwa wanawake wanaokutwa na misukosuko katika ndoa zao.
"Filamu ya Kua Uyaone ni filamu yangu ya kwanza kuandaa na kuigiza nikiwa mhusika mkuu. Inazungumzia maisha yangu halisi ya ndoa," alisema.
"Inaonyesha jinsi nilivyoteseka na kumpoteza mume, nimefanya hivi ili kuwatia nguvu wanawake wenzangu."
Dometria ambaye ni pacha wa msanii wa filamu nchini Dotnata, anasema kuwa amekuwa akiandika hadithi za filamu kwa muda mrefu, lakini alikuwa akishiriki sehemu fupi fupi tu za filamu zilizoandaliwa na pacha wake huyo ambaye ni Doto.
Msanii huyo ameamua kurekodi filamu hiyo inayoitwa 'Kua Uyaone' kama faraja kwa wanawake wanaokutwa na misukosuko katika ndoa zao.
"Filamu ya Kua Uyaone ni filamu yangu ya kwanza kuandaa na kuigiza nikiwa mhusika mkuu. Inazungumzia maisha yangu halisi ya ndoa," alisema.
"Inaonyesha jinsi nilivyoteseka na kumpoteza mume, nimefanya hivi ili kuwatia nguvu wanawake wenzangu."
Dometria ambaye ni pacha wa msanii wa filamu nchini Dotnata, anasema kuwa amekuwa akiandika hadithi za filamu kwa muda mrefu, lakini alikuwa akishiriki sehemu fupi fupi tu za filamu zilizoandaliwa na pacha wake huyo ambaye ni Doto.
0 comments:
Post a Comment