Friday, July 13, 2012

.......BADRA AKIMBILIA KWENYE MZIKI.....

STAA wa filamu za Swahiliwood, Latifa Idabu Badra, ameamua kufungua kipaji chake kwa upande mwingine katika kuimba na tayari amefanikiwa kurekodi wimbo alioupa jina la 'Twende Sawa'.

Badra ameiambia Mwanaspoti kuwa yeye tangu awali alikuwa akiimba, lakini kutokana na mazingira ya kidini ya nyumbani kwao alishindwa kufanya hivyo mapema.

Toka kitambo nilikuwa nikiimba labda hata ningetoka katika uimbaji kabla hata ya filamu, lakini kutokana na wazazi wangu kuwa waswalina haikuwa rahisi," anatoboa siri.

"Muziki ninaoimba ni Hip Hop ambao unaonekana kama ni muziki wa kihuni, kwa sababu ni kitu ambacho ninacho rohoni kwangu sina budi kukifanya sasa."

Msanii hiyo anasema kuwa kuna wakati ambao watoto hupoteza vipaji vyao kwa sababu ya wazazi kushindwa kubaini uwezo na vipaji vya watoto husika, yeye anashukuru kuwa kwa sasa anaweza kufanya jambo lolote katika kuibua vipaji vyake kwani amekuwa ni mtu mwenye maamuzi yake ana maisha yake ambayo si tegemezi tena.

0 comments:

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Grants For Single Moms