Madaktari na wauguzi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakiisukuma gari iliyokuwa imempaki Dk. Stevan Ulimboka.
Madaktari na Wauguzi wa Muhimbili wakiwa wamesimama huku wakizungumzia hali iliyompaka mwenzao.
Hakuna kazi iliyokuwa ikifanyika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakati Dk. Ulimboka akifikishwa hospitalini hapo.
Wanahabari wakitafuta taswira.
Picha zote na matukio michuzi blog
...KAMA KOVA AZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI...
Kamanda wa
polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Kamanda Suleiman Kova amezungumza na
waandishi wa habari kuhusu tukio hilo la utekaji nyara na kujeruhi lililompata
kiongozi mgomo wa Madaktari Steven Ulimboka anayedaiwa kutekwa na watu watano
wakati akipata kinwaji katika klabu ya Leaders Kiondoni jijini Dar es salaam.
Kamanda Kova
amesema Ulimboka aliokotwa na msamaria mwema ambaye hakutaka kumtaja jina lake
kiusalama na kutoharibu upelelezi kuwa msamaria mwema huyo alimuokota Ulimboka
katika msitu wa Mabwepande na kutoa taarifa kituo cha polisi cha Bunju, ambapo
polisi aliyekuwa zamu alichukua maelezo yake na baadae Steven Ulimboka kuletwa
katika hospitali ya taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.
Kamanda Kova amesema
jeshi la Polisi Kanda Maalum limeunda jopo maalum kwa ajili ya uchunguzi na
upelelezi wa tukio hilo la utekaji nyara, kwani ni tukio la kwanza kutoke
nchini, ameongeza kwamba wahusika wote watakaobainika kuhusika na tukio hilo
wachukuliwa hatua za kisheria na sheria itafuata mkondo wake ili kukomesha
matukio mengine kama hayo
0 comments:
Post a Comment