MWANANADADA
tishio katika kupamba video za wanamuziki mbalimbali nchini Agnes Gerald
maarufu kama Agnes Masogange ameweka wazi kuchukizwa na tabia ya mastaa wa kike
wa bongo muvie kuwadharau wasichana 'wanaouza sura' (video Queen). Mwanadada
huyo mwenye umbo la utata, ambaye kuzitendea haki fedha anazolipwa kwa 'kuuza
sura' alisema kwamba tabia hiyo iliyokithiri imekuwa ikonekana mara nyingi
wanapokutana katika mikusanyiko mbalimbali ikiwemo kwenye kumbi za starehe
ambapo mastaa wa bongo movie huwaona video Queen hao kuwa si lolote.
"nawashangaa sana na hizi tabia zao kwani kazi ni kazi tu kama ilivyokwao
katika kuigiza, kikubwa ni kila mtu anakula kwa jasho lake...nashangaa
wanavyotunyanyapaa tunapokutana klabu,"alisema.
0 comments:
Post a Comment