Warembo watakaoziwakilisha Nchi zao katika mashindano ya Miss East Africa
mwaka huu wanaendelea kupatikana kutoka katika Nchi mbalimbali zinazoshiriki
mashindano hayo.
Mrembo mwingine aliyeingia fainali ni Miss Lula Teklehaimanot (19) kutoka
Nchini Ethiopia ambae alipatikana mwishoni mwa wiki baada ya kuwashinda warembo
wenzake waliojitokeza kutaka kuiwakilisha Ethiopia katika fainali hizo.
Miss Lula Teklehaimanot ana urefu wa 1.79m na uzito wa 52kg ni mwanafunzi
wa mwaka wa kwanza katika chuo cha St. Merry University cha jijini Addis Ababa,
Ethiopia ampapo anasomea degree ya Marketing
Pia Mrembo huyo ni miongoni mwa wanamitindo maarufu wanaochipukia kwa
kasi Nchini Ethiopia.
Fainali za mashindano ya Miss East Africa 2012 zitafanjika tarehe 07
mwezi September mwaka huu jijini Dar es salaam
0 comments:
Post a Comment