Friday, May 11, 2012

.....JB NUSURA AUAWE NA MAJAMBAZI....AELEZEA JINSI ILIVYOKUWA....


MCHEZA filamu anayetamba kwenye ‘game,’ Jacob Steven ‘JB’ (pichani) hivi karibuni alinusurika kuuawa na majambazi waliovamia Pub ya msanii mwenzake, Aunt Ezekiel iliyopo eneo liitwalo Gereji Mwananyamala jijini Dar.
Akizungumza na Ijumaa, JB alisema kuwa baada ya majambazi hao kuvamia katika pub hiyo saa 5.30 usiku, hakuwastukia kama walikuwa wahalifu bali alidhani ni wateja wa kawaida.
“Mimi sikuwashitukia kama wale watu walikuwa majambazi, ila baada ya kutoa bastola na kutuamuru tulale chini na tutoe kila kitu nikajua kimenuka, nikatimua mbio ambazo sijawahi kukimbia licha ya mwili wangu huu,” alisema JB.
Aliongeza kuwa, wakati akitimua mbio aliwasikia watu wakimuaru asimame lakini hakutii hadi alipofika Kituo cha daladala cha Komakoma ndipo alisimama na kumshukuru Mungu kwa kumnusuru na kifo.

0 comments:

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Grants For Single Moms