Friday, May 4, 2012

.......JAMAA YUKO JUU ILE MBAYA....

RAMSEY Nouah ametamka hadharani kwamba hakuna jinsi utakavyoitaja fani ya filamu Nigeria uache kumgusa, lakini anafikiria kukaa pembeni kabla hajachuja.

Msanii huyo alisema; "Najua mashabiki wangu watataka kuniona siku zote kwenye runinga, lakini kama ilivyo kawaida, lazima ung'atuke ukiwa bado unapendwa.

Najua nimefanya mambo makubwa sana kwenye hii tasnia, hakuna jinsi utakavyotaja jina Nollywood uache kunitaja."

"Nitakuwa naigiza hapa na pale lakini kidogo sana, nitakuwa nafanya sana mambo ya uongozaji, kuna kipindi kirefu sasa sijaonekana kwenye runinga kwa sababu sitaki kufanya kazi ambazo hazina viwango.

"Sitaki kufanya kazi ilimradi, nataka kuhusishwa na filamu zenye viwango na heshima kwenye hii fani."




0 comments:

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Grants For Single Moms