Olomide akiwa ofisini kwake
Anaitwa Mopao Mokonzy Baba Didie Stone Koffi
Charles Olomide ambaye hivi karibuni amesaini mkataba mwingine na Bia ya SKOL
wa kumdhamini kwa miaka miwili ambapo kampuni hiyo itagharaia show zake na
kuwalipa mishahara wanamuziki wake.
Koffi kwa sasa amezidisa show zake za barani
afrika na kuimarisha zile za Kongo Kinshasa ikiwa ni matokeo ya wanaharakati wa
Congo wanaojulikana kama Banakongo au Lecombatant ambao wameongoza kufanya fujo
kwenye show za wanamuziki wote ambao walikuwa wakimsupport Rais Kabila kwenye
kampeni ambapo Koffi alitunga wimbo kwa ajili ya kuhamasisha wananchi wa Congo
kumchagua Kabila ambaye alishinda uchaguzi huo.
Koffi ambaye amesemwa anataka kugombea
uchaguzi ujao kwa nafasi ya Ubunge ingawa mwenyewe aliwahi kukanusha hilo
lakini watu waliokaribu naye wanasema anampango huo. Hata hivyo wachunguzi
wengine wanasema haitakuwa rahisi kwa Koffi kugombea kwa vile si raia wa Kongo
akisemwa kuwa anatokea Gabone na wakati mwingine inasemwa anatokea Congo
Brazaville na mmoja wa wazazi wake ndio Mkinshasa.
0 comments:
Post a Comment