Friday, April 27, 2012

......KOFI OLOMIDE ASAINI MKATABA MNONO..........

Olomide akiwa ofisini kwake

Anaitwa Mopao Mokonzy Baba Didie Stone Koffi Charles Olomide ambaye hivi karibuni amesaini mkataba mwingine na Bia ya SKOL wa kumdhamini kwa miaka miwili ambapo kampuni hiyo itagharaia show zake na kuwalipa mishahara wanamuziki wake.
Koffi kwa sasa amezidisa show zake za barani afrika na kuimarisha zile za Kongo Kinshasa ikiwa ni matokeo ya wanaharakati wa Congo wanaojulikana kama Banakongo au Lecombatant ambao wameongoza kufanya fujo kwenye show za wanamuziki wote ambao walikuwa wakimsupport Rais Kabila kwenye kampeni ambapo Koffi alitunga wimbo kwa ajili ya kuhamasisha wananchi wa Congo kumchagua Kabila ambaye alishinda uchaguzi huo.
Koffi ambaye amesemwa anataka kugombea uchaguzi ujao kwa nafasi ya Ubunge ingawa mwenyewe aliwahi kukanusha hilo lakini watu waliokaribu naye wanasema anampango huo. Hata hivyo wachunguzi wengine wanasema haitakuwa rahisi kwa Koffi kugombea kwa vile si raia wa Kongo akisemwa kuwa anatokea Gabone na wakati mwingine inasemwa anatokea Congo Brazaville na mmoja wa wazazi wake ndio Mkinshasa.

0 comments:

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Grants For Single Moms