KIM
Kardashian amejipanga kujiongezea uwanja mwingine wa kujionyesha kwani amesema
ndani ya miaka mitano ijayo anataka kutimiza ndoto yake ya kuingia katika
siasa.
Katika kipindi cha Keeping up With Kardashians, Kim amesema anataka kugombea Umeya wa Jiji la Glendale katika uchaguzi ujao.
Kim, mwenye umri wa miaka 31, alimwambia ndugu yake Kloe kuwa anatarajia kununua nyumba katika mji huo ili waanze kuishi huko na kujitengenezea mazingira ya ushindi.
Hata hivyo, Kim amekosolewa kwa kutaka kujiingiza kwenye siasa wakati hazijui hata kidogo. Inaelezwa kuwa hakuna nafasi ya Umeya katika Jiji la Glendale. Jiji hilo linaongozwa na wajumbe watano wa Halmashauri.
Katika kipindi cha Keeping up With Kardashians, Kim amesema anataka kugombea Umeya wa Jiji la Glendale katika uchaguzi ujao.
Kim, mwenye umri wa miaka 31, alimwambia ndugu yake Kloe kuwa anatarajia kununua nyumba katika mji huo ili waanze kuishi huko na kujitengenezea mazingira ya ushindi.
Hata hivyo, Kim amekosolewa kwa kutaka kujiingiza kwenye siasa wakati hazijui hata kidogo. Inaelezwa kuwa hakuna nafasi ya Umeya katika Jiji la Glendale. Jiji hilo linaongozwa na wajumbe watano wa Halmashauri.
0 comments:
Post a Comment