Monday, April 23, 2012

...KESI YA LULU KUSOMWA TENA MEI SABA........


Mahakama ya hakimu mkazi KISUTU jijini Dar es Salaam leo imeahirisha kesi ya tuhuma za mauaji inayomkabili ELIZABETH MICHAEL ‘LULU’ dhidi ya aliyekuwa mwana filamu mahiri Marehemu STEVEN KANUMBA.

Wakili wa Upande wa Serikali ELIZABETH KAGANDA akizungumza mahakamani hapo amedai Upepelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kwamba kesi hiyo itatajwa tena mei 7 mwaka huu.

Umati mkubwa ulijitokeza katika mahakama hiyo kwa lengo la kufuatilia mwenendo mzima wa kesi hiyo ambayo imevuta hisia za watu wengi hapa nchini.
Hii ni mara ya Pili kwa ELIZABETH MICHAEL kupandishwa Kizimbani kosa la mauaji ya mwana filamu huyo mnamo April 7 mwaka huu eneo la Sinza Vatican Jijini Dar es Salaam.

0 comments:

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Grants For Single Moms