MWIGIZAJI
nyota wa Swahiliwood, Ruth Suka Mainda amedai kukumbwa na usumbufu kutoka kwa
wadau na wapenzi wa filamu baada ya kupigiwa simu nyingi huku kila mpiga simu
akitaka kujua kuhusu ujauzito wake.
Mainda amesema, tukio hilo limejitokeza hivi karibuni kwa baadhi ya watu kumpigia simu wakitaka kujua kama kweli ni mjamzito.
Ninasumbuliwa sana na watu wakitaka kujua kama kweli mimi ni mjamzito, na ukichelewa kumjibu mtu ukiwa umeduwaa, swali linalofuata kabla hata ya kujibu anakuuliza je, baba wa mtoto ni nani? Jibu ni kwamba, mimi si mjamzito bali ni filamu tu, anasema Mainda.
Mainda anafafanua kuwa, wengi wanampigia simu kutokana na picha alizopiga akiwa anarekodi filamu yake mpya ya Mke Mwema ambayo kaigiza kama mama mjamzito mwenye matatizo na picha hizo kuchukuliwa na watu ambao wanatangaza kuwa yeye ni mjamzito.
Mainda amesema, tukio hilo limejitokeza hivi karibuni kwa baadhi ya watu kumpigia simu wakitaka kujua kama kweli ni mjamzito.
Ninasumbuliwa sana na watu wakitaka kujua kama kweli mimi ni mjamzito, na ukichelewa kumjibu mtu ukiwa umeduwaa, swali linalofuata kabla hata ya kujibu anakuuliza je, baba wa mtoto ni nani? Jibu ni kwamba, mimi si mjamzito bali ni filamu tu, anasema Mainda.
Mainda anafafanua kuwa, wengi wanampigia simu kutokana na picha alizopiga akiwa anarekodi filamu yake mpya ya Mke Mwema ambayo kaigiza kama mama mjamzito mwenye matatizo na picha hizo kuchukuliwa na watu ambao wanatangaza kuwa yeye ni mjamzito.
0 comments:
Post a Comment