Tuesday, March 6, 2012

.......RIHANNA YUKO SINGLE LAKINI..........


Japokua watu wengi walikua wanategemea kwamba kwenye interview ya kwanza atakayoifanya Rihanna baada ya kusherehekea birthday yake na mpenzi wake wa zamani Chris Brown, angemzungumzia Chris Brown au kutoa majibu tofauti kuhusu uhusiano wake wa kimapenzi, ishu imegeuka tofauti.
Baada ya kualikwa kwenye show ya Jonathan Ross London Uingereza, Rihanna aliwashangaza watu kuhusu jibu alilolitoa kuhusu msimamo wake wa kimapenzi sasa hivi kwani wiki moja iliyopita baada ya Chris Brown kutokea kwenye birthday party yake na wawili hao kuonekana wakikaa kwenye mapozi ya mahaba, wakiwa wameshikana mikono, kukumbatiana mara kwa mara pamoja na kisses kuhusika, wengi walisema kazi imekwisha…… yani Chris Brown amerudiana na Rihanna, na walipotoa wimbo wao pamoja, ndio hizo habari zikazidi kukolezwa kabisa.
Sasa turudi kwenye show ya Jonathan Ross, kilichotokea ni kwamba Rihanna mwenyewe kwa mdomo wake, amekubali kwamba bado yuko kwenye maisha ya upweke, hana mpenzi kwa sasa, na anamiss kuwa kwenye mapenzi kwa sababu ameyachoka maisha ya upweke.
RiRi amesema ana hamu ya kumpata mtu ambae atamridhisha kimapenzi, hicho ndio kitu pekee anachokubali kwamba ana kimis sana kwa sasa, anataka aina ya mwanaume atakaempata awe ametulia na mcheshi.
Wengi walidhani angekubali kwamba karudiana na chris brown, sijashangaa sana imekuaje Jonathan hakumuuliza kuhusiana na stori za kurudiana na Chris Brown, inawezekana kabla hawajaanza interview labda Rihanna aliomba hiyo ishu isizungumziwe manake ingemuharibia zaidi watu wengi wangemshangaa kurudiana na mwanaume ambae alimpiga na kesi yao ilikua kubwa.

0 comments:

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Grants For Single Moms