Wednesday, March 28, 2012

........CHIDI BENZ AMJINBU AFANDE SELLE ......


Pamoja na kwamba watu wanaona ni beef imeanza  kati ya Afande Selle na Chidi Beenz, Chidi Beenz amesema wiki moja kabla ya Afande Selle kumdiss on East Africa Radio, alikua amepanga kumtafuta kwa ajili ya kumpa shavu la single yake mpya anayotaka zisikike sauti za Mwana FA na Afande Selle.
Amesema “wiki moja kabla nilikua niko na Tippo wa Zizzou tulikua tunaongelea ngoma flani hivi niliwahi kurekodi nikaanza kurekodi chorus alafu nikaiacha, nikamtumia Mwana FA aandike verse yake pia ngoma inaitwa Mani, Zizzou akaniambia ukimtumia na Afande itakua poa anaweza kuandika kitu kizuri sana alafu hajasikika siku nyingi itakua safi, nikasema kweli bwana hata mimi sijamsikia Afande zamani itabidi nikifika Dar  nimtafute kwenye simu”
Mfalme wa Ilala amesema “yani juzi nimesikia Afande ananidiss nikacheka, nikaona Afande juzi tu tumekutana kwenye show ya CLOUDS nimemuona Afande anazurura peke yake nikamuita nikiwa na Fid Q, Prof J, FA na wengine nikamwambia Afande njoo tupige picha mpaka leo ninayo, watu walicheka wakafurahi pia, sasa from no where Afande amenidiss mimi wakati mi sijawahi kusema chochote kibaya kuhusu yeye”
Kwa kumalizia CHIDI amesema “sijaufuta huo mpango wa kufanya kolabo na Afande Selle, namfahamu ni mtu mmoja anabadilika kwa haraka sana na kuomba sana msamaha, wazo la kufanya nae kolabo bado ninalo na kama atakubali tutarekodi, hakuna sababu ya kugombana wala kusemana”
Chanzo cha haya yote ni wakati Afande Selle alipofananisha kitendo cha mwimbaji DITTO kuondoka kwenye kundi lake la WATU PORI na kwenda LA FAMILIA ya CHIDI BENZ, sawa na kuondoka MANCHESTER UNITED kwenda WOLVERMPTON.
Akiamplfy na millardayo.com march 26 2012, Chidi alikanusha taarifa kwamba atamteka na kumpiga Afande Selle vilevile akamuonya JAY MOE kutoingilia chochote kati yake na Afande Selle huku akisisitiza kwamba “hata nilivyomuona na Jay Moe kwenye ile interview namuona Jay Moe, Jay Moe ni nini bwana vitu anaongea Jay Moe pale na Afande wote kabila moja, ni watu ongea sawa”
Chidi amesema hatofanya chochote kama ikitokea akakutana na Afande Selle sehemu yoyote, atamsalimia na kuendelea na shughuli nyingine.

0 comments:

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Grants For Single Moms